SANTOS ACHAGULIWA TENA KUONGOZA CHAMA TAWALA ANGOLA


santo
Jose Eduardo dos Santos amekuwa madarakani kwa miaka 36
Rais wa Angola, Jose Eduardo dos Santos aliyeongoza kwa miaka 36 amechaguliwa tena kuwa kiongozi wa chama tawala cha MPLA.
Uchaguzi wa bunge unatarajiwa kufanywa mwaka ujao, na kiongozi wa chama kinachoshinda ndiye anayekuwa rais.
Rais dos Santos alisema awali mwaka huu, kwamba ataondoka madarakani mwaka wa 2018, lakini ameshawahi kutoa ahadi kama hizo kabla.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 73, analaumiwa kuwa amekusanya madaraka mengi na mali, kwenye mikono ya familia yake na washirika wake wakubwa kisiasa.
Chanzo: BBC
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment