Ikiwa
imepita mwezi mmoja na nusu tangu aliyekuwa kiungo wa Juventus, Paul
Pogba kujiunga na timu yake ya zamani, Manchester United kwa kitita cha
Euro 105, wakala wa mchezaji huyo, Mino Raiola amefunguka kuhusu siri
ambayo watu wengi walikuwa hawaijui.
Raiola
amesema kuwa kabla ya kocha Mourinho kumsajili akiwa Pogba akiwa
Manchester Unite, alianza kumhitaji Pogba tangu alipokuwa akiifundisha
Chelsea lakini alishindwa kujiunga kutokana na makubalianoo yaliyokuwepo
ya Pogba kuisaidia kwanza Juventus kushinda kombe la Ligi ya Mabingwa
Ulaya (UEFA Champions League).
“Paul
alikuwa aondoke [Juventus] mwaka jana sababu ya Jose Mourinho wakati
akiwa Chelsea, kweli walikuwa wakimhitaji,” alisema Raiola na kuongeza.
“Lakini
mimi na Juventus tulikuwa na makubaliano, washinde ubingwa wa ligi na
kombe la mabingwa Ulaya, na baada ya hapo angeondoka”


0 comments :
Post a Comment