NDESAMBURO AMTOLEA UVIVU JPM,AMSHANGAA KWA KUIPENDELEA CCM KATIKA TEUZI ZAKE !!!


Mwanasiasa mkongwe, Philemon Ndesamburo amedai hatua ya Rais John Magufuli kuteua wakurugenzi wa halmashauri nje ya mfumo wa Serikali, umewavunja moyo watumishi wengine.


Ndesamburo ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Moshi Mjini (2000-2015), alisema mfumo huo ulikuwa ukiwajenga watumishi kutoka madaraja ya chini hadi uandamizi, hao ndiyo walikuwa wakiteuliwa.

Julai 7, Rais Magufuli aliteua wakurugenzi 185 kati yao 65 ndiyo walioteuliwa kutoka orodha ya zamani ya wa kurugenzi na 120 ni wapya.
 
Kati ya hao wapya, wapo walioteuliwa miongoni mwa makada wa CCM walioshindwa kura za maoni ndani ya chama hicho 2015 na wengine wakitoka nje ya mfumo wa utumishi wa umma.

Ndesamburo alidai hatua ya Rais kuteua makada wa CCM nje ya mfumo kushika wadhifa huo, utaziyumbisha halmashauri nyingi kwani wengi hawajui namna ya kushughulikia madokezo.
 
“Kwenye baadhi ya halmashauri hao ambao walionekana hawawezi kuwa promoted (kuteuliwa), ndiyo wanaowafundisha wakurugenzi wapya. Hapa kidogo Rais wetu alichemka,” alidai Ndesamburo.

Akizungumza katika mahojiano maalumu  jana, Ndesamburo alidai nafasi za uteuzi kama za wakuu wa mikoa na wilaya, Rais angeweza kuteua makada wa CCM lakini siyo ukurugenzi.
CHANZO :Swahiba news
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment