SERIKALI YAFUNGA NA KUZIFUTA SHULE 40..!!!



WIZARA ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imezifuta shule za awali, msingi na sekondari nchini ambazo hazijasajiliwa zaidi ya 40 kuanzia Julai mwaka jana.

 
Awali kuanzia Julai hadi Desemba mwaka jana, waligundua kuwepo kwa shule 35 zisizosajiliwa na kuzifuta, jambo lililofanya kutangaza shule zote ambazo hazijasajiliwa kujisalimisha ili kusajiliwa.

Kaimu Mkurugenzi wa Usajili wa Shule katika wizara hiyo, Khadija Mcheka alisema Mei mwaka huu baada kuzipa miezi
 miwili shule ambazo hazijasajiliwa kufanya hivyo, walizifungia shule nyingine 12.

Alitaja shule zilizofungiwa kwa kuendesha shughuli zake bila usajili kuwa ni shule za awali na msingi za Must Lead ya mkoa wa Pwani, na za mkoa wa Dar es Salaam ni Brainstorm, Pax, Lassana, Grace, Rose Land, Julius Raymod, St Thomas, Mary Mother of Mercy, Noble Sinkonde, Immaculate Heart of Mary, St Columba, Corner stone, Dancraig, Mwalimu Edward Kalunga, Edson Mwidunda, Gisela, Kingstar, St Columba awali, Bilal Muslim, Thado, Hocet , Elishadai, Lawrance Citizen, Comrade, Dar Elite Preparatory na Golden Hill Academy na Hekima.

Nyingine ni Pwani Islamic, St Kizito na Rwazi Encysloped za Kagera, Dancraig na Qunu za Pwani, Hellen’s ya Njombe, Joseph ya Arusha, Samandito na Maguzu za Geita. Alizitaja shule za Sekondari zilizofungiwa kwa sababu hiyo kuwa ni Hananasif, Elu, Hocet, Safina za Dar es Salaam na Namnyaki ya Iringa.

Aidha, Shule ya Fountain Gate ya jijini Dar es Salaam imefungiwa kwa kuendesha bweni bila kibali.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment