VIONGOZI WA CHAMA KIKUU CHA UPINZANI TANZANIA-CHADEMA WAENDA UJERUMANI KUJIFUNZA..!!!

Ujumbe wa Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ukiongozwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Vincent Mashinji  umewasili katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya siku 7 katika nchini hiyo.


Taarifa iliyotolewa na chama hicho , imewataja walioambatana katika ujumbe huo unaojumuisha watu 10, kuwa ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Bara) John Mnyika, Mjumbe wa Kamati Kuu Prof. Mwesiga Baregu, Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho, Tundu Lissu, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itifaki na Mambo ya Nje, John Mrema, Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama, Benson Kigaila.

Pia imewataja wengine waliopo kwenye msafara huo kuwa ni, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa CHADEMA, Zanzibar Zeudi Mvano Abdillahi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Ruth Mollel, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha, Cecilia Paresso na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ilala Anatropia Theonest.

Katika ziara hiyo ya kikazi iliyoanza Septemba 18, ujumbe huo mbali ya kufika Wizara ya Mambo ya Nje ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, kwa ajili ya mazungumzo, pia utafika Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya nchi hiyo.

Aidha utakutana na kufanya mazungumzo na Wabunge wa Bunge la Shirikisho la Nchi ya Ujerumani na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini humo, kujadiliana na kubadilishana uzoefu wa masuala mbalimbali, hususan kiuchumi na kisiasa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment