Ikiwa
imesalia masaa machache kabla ya kuanza kutumia vumbi kwa mchezo wa
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), kati ya Mbeya City ambayo inaikaribisha
Simba, na wenyeji Mbeya City ikianza kuwatupia lawama Simba kuwa
inawafanyia hujuma ili ishinde, Simba nao wamewajibu.
Simba
kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe
amesema Simba inafanya maandalizi kwa ajili ya mchezo na hakuna hujuma
yoyote ambayo wanaifanya na kama Mbeya City watakuwa na hofu na hilo
basi waende katika vyombo vinavyohusika.
“Kama
kuna malalamiko waende kunapohusika, sisi kama Simba tumefika Mbeya
salama na tunajiandaa kwa ajili ya kwenda kupambana katika dakika 90 na
kupata alama tatu tunazozihitaji,
“Mpira
unachezwa hadharani na unakuwa na wachezaji 11, mimi nadhani haya ni
maneno ya kukuza mchezo lakini matokeo yatajulikana baada ya mchezo,
Mbeya City ni timu nzuri na mara nyingi wamekuwa wakitusumbua,” amesema
Hans Poppe na kuongeza.
“Tuna
timu nzuri na hatujapoteza mechi hata moja, sisi kama uongozi wa timu
tuna kazi ya kuhakikisha tunapata alama tatu kila mchezo ili tuendeleze
rekodi yetu ya kutokufungwa katika michezo yetu”


0 comments :
Post a Comment