TAIFA STARS YAFANYA MAZOEZI YA MWISHO,TAYARI KUWAVAA ZIMBABWE KESHO.


Siku ya Jumapili November 13,2016 timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ itashuka dimbani kucheza na wenyeji Zimbabwe mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaochezwa kwenye uwanja wa Taifa wa Harare mjini Harare.
Mchezo huo utachezwa majira ya saa tisa alasiri kwa saa za Zimbabwe wakati Tanzania itakuwa saa kumi jioni kwa saa za Afrika Mashariki na utakaoneshwa na kituo cha Televisioni ya Taifa ya Zimbabwe (ZBC) na hapa nyumbani wataungana na kituo cha Televisioni cha Azam TV.
Wakiwa chini ya kocha Mkuu Boniface Mkwasa kikosi chote kimefanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Harare na tayari kwa vita hiyo ya Kesho na ushindi wa kesho utakuwa na faida ya kuipandisha Tanzania katika viwango vya FIFA.
taifa1
Mchezaji wa timu ya Tanzania Mbwana Samatta ambaye pia anachezea timu ya Genk ya Ubelgiji akiwa na mchezaji mwenzake Thomas Ulimwengu wakijiandaa kwa mazoezi mjini Harare nchini Zimbabwe tayari kwa mchezo wao na timu ya Taifa ya Zimbabwe jumapili.
taifa2
wachezaji wa timu ya Taifa Taifa Stars wakijiandaa kwa mazoezi.
taifa3 taifa4
Mchezaji Thomas Ulimwengu akibeba majiya kunywa kwenye toroli   kwa ajili kunywa wakati wa mazoezi  ya timu hiyo.
taifa5
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa taifa Stars Boniface Mkwasa akijadiliana jambo na makocha wenzake.
taifa6
Mazoezi yakiendelea.
taifa7 taifa8 taifa10
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment