WATU
 wawili wamekufa huku wengine wanne wakijeruhiwa baada ya majambazi 
walio na silaha kuvamia mgodi wa dhahabu wa Nholi uliopo wilaya ya Bahi 
mkoani Dodoma.
Majambazi hao wanadaiwa kupora dhahabu, fedha na mali nyingine na kuwavua watu nguo na kuondoka nazo.
Mganga
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Charles Kiologwe alikiri kupokelewa kwa 
miili ya watu wawili hospitalini hapo na majeruhi wanne.
Alisema
 mwili mmoja upo katika hali mbaya. Waliofariki dunia katika tukio hilo,
 walitajwa kuwa ni Lukumale Membo na mwingine aliyefahamika kwa jina 
moja la Hamisi.
Kwa
 mujibu wa Muuguzi Msaidizi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, 
Melisiana Danford, maiti hao na majeruhi walipokelewa hospitalini hapo 
saa 6 usiku kuamkia jana mara tu baada ya kutokea kwa tukio hilo. 
Majeruhi katika tukio hilo ni Sunday Undi (49), Lawrence Mhagama (35) , 
Maila Mchele (44) na Sophia Sayuni (37).
Wakizungumza
 katika wodi namba moja ambako wamelazwa, majeruhi hao walisema 
walivamiwa na majambazi, ambao baadaye waliwapiga risasi na kusababisha 
vifo vya watu wawili na wengine kujeruhiwa.
Lawrence
 Mhagama ambaye amepigwa risasi mguu wa kushoto, alisema amekuwa 
akiendesha shughuli za uchimbaji mdogo kwenye mgodi huo. Alisema siku ya
 tukio majira ya saa mbili usiku akiwa ndani, alisikia milio ya risasi 
nje na alipojaribu kutoka, alipigwa risasi ambayo ilimjeruhi mguuni.
“Chanzo
 cha tukio kwa kweli sikijui ila majambazi walituvamia , mimi ni mgeni 
eneo hilo nilikwenda kwa ajili ya kazi ya mgodi, nimepigwa risasi mguuni
 ambapo mpaka sasa bado ninayo mwilini, wanasema wataniruhusu nikipata 
nafuu na baadaye wataangalia uwezekano wa kuitoa risasi hiyo,” alisema.
Alisema majambazi hao, walipora mali nyingi ambapo waliwavua watu nguo na kuondoka nazo huku wakiacha watu uchi.
Majeruhi
 mwingine aliyelazwa wodi namba moja, Sunday Undi, alisema walivamiwa na
 majambazi hao majira ya saa mbili kasorobo usiku wa kuamkia juzi, 
wakiwa kwenye kioski cha Maila Mchele, wakipata vinywaji na kuendelea na
 mazungumzo.
“Tulivamiwa
 tukasikia tunaambiwa tuko chini ya ulinzi, kwa vile lilikuwa ni tukio 
la kushtukiza tukawa tunashangaa, wakapiga risasi juu ikabidi tuingie 
ndani ya kibanda kile baada ya muda tukajikuta watu saba tukiwa chini ya
 kitanda,” alisema.
Alisema majambazi hao waliwaamrisha watoke na kuwaambia kila mtu atoe alichonacho na aliyekuwa akikataa, aliamriwa kuvua nguo.
“Walininyang’anya
 fedha na simu, wakatuvua na suruali wakaondoka nazo, mimi binafsi 
wamenipora Shilingi milioni mbili nilizokuwa nazo,” alisema.
Alisema
 majambazi hao walikuwa zaidi ya wanne na walikuwa wamevalia kininja. 
Alisema mtu aliyejaribu kuwatazama usoni, alikuwa akipigwa risasi. 
Majeruhi mwingine katika tukio hilo, Maila Mchele ambaye amelazwa wodi 
hiyo akiwa hajitambui, amejeruhiwa vibaya.
Inadaiwa
 alipigwa risasi tumboni na kutokea upande wa pili. Majeruhi wa nne, 
Sophia Sayuni (37) amelazwa wodi namba 10 hospitalini hapo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alipohojiwa kuhusu tukio hilo, alisema atalitolea ufafanuzi baadaye.



0 comments :
Post a Comment