Rais Magufuli Ateua Mwenyekiti Wa Bodi Mamlaka Ya Masoko Ya Mitaji Na Dhamana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli,  amemteua Dkt. John Kedi Mduma kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. John Kedi Mduma umeanza tarehe 23 Februari, 2017.

Dkt. John Kedi Mduma ni Mhadhiri Mwandamizi, Idara ya Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Dkt. John Kedi Mduma anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bi. Grace Rubambey ambaye amemaliza muda wake.
***

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment