Mbunge
wa Kigoma Mjini ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto
Kabwe amemkingia kifua Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na kusema
kuwa anaamini Mbunge huyo wa Hai hajawahi kujihusisha na dawa za kuleva
kwa namna yoyote
Zitto
ambaye ameambatana na Mbowe katika mkutano wake na wanahabari leo mjini
Dodoma, amesema kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul
Makonda kumtaja Mbowe katika sakata la dawa za kulevya ni sawa na
kutangaza vita na chuki dhidi ya chama hicho.
Amesema
kuichafua CHADEMA ni sawa na kuuchafua upinzani hivyo na yeye hawezi
kukaa kimya kuona upinzani ukishambuliwa, na ndiyo sababu ya kuongeza
nguvu kwa kuungana naye.



0 comments :
Post a Comment