Baada ya kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwa taarifa zinazodaiwa kutoka kwa Rais wa TFF Jamal Malinzi kuwa ametengua maamuzi ya kamati ya saa 72 kuipaSimba point tatu dhidi ya Kagera Sugar katika kikao chao cha juzi April 13, Rais wa TFF Jamal Malinzi amekanusha taarifa hizo.

Rais wa TFF Jamal Malinzi

Jamal Malinzi amekanusha taarifa feki zinazosambaa katika mitandao ya kijamii zikidai kuwa yeye ametengua maamuzi ya kamati ya saa 72 ya kupewa point tatu kwaSimba, Malinzi amenadika ujumbe kupitia ukurasa wake wa twitter “Taarifa zinasombaa kwenye mitandao kuwa nimetengua maamuzi ya kamati ya uendeshaji wa ligi si za kweli.TFF ina taratibu zake za kutoa maamuzi”

Taarifa feki iliyokuwa ikisambazwa katika mitandao ya kijamii kuhusu Jamal Malinzi
.
.
About Unknown
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.


0 comments :
Post a Comment