Taarifa Ya Ajali Treni Na Dala Dala

Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kutokea ajali ya basi la abiria/daladala (T 435 DGG) kutoka Gongo la Mboto kwenda Mnazi Mmoja kuigonga treni ya Pugu leo Aprili 19, 2017 saa 11 alfajiri katika makutano ya reli na barabara ya Nkurumah jijini Dar es Salaam.



Majeruhi wa ajali ni 23 , wanane wapo hospitali ya Amana na waliobakia 15 wapo Hospitali ya Taifa Muhimbili MOI watatu kati yao ni mahututi. Taarifa zaidi itatolewa kuhusu ajali hiyo.



Hata hivyo treni ya Pugu inaendelea na huduma zake kwa kufuata ratiba.



Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL



Nd. Focus Sahani,

Dar es Salaam,

Aprili 19, 2017.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment