Mahakama ya Kampala leo imemtoza mbunge wa Manispaa ya Arua Ibraham Abiriga faini ya Sh40,000 kwa kosa la kujisaidia haja ndogo hadharani.
Amepewa adhabu hiyo baada ya kupatikana na kosa la kujisaidia haja ndogo katika ukuta wa uzio wa wizara ya fedha. Mbunge huyo alikiri kosa na akaamriwa kulipa faini hiyo au kutumikia kifungo cha wiki mbili jela. Abiriga amelipa faini hiyo na akaruhusiwa kuondoka.
Upande wa mashtaka uliiambia mahakama kwamba Septemba 25, 2017 katika barabara ya Kyaggwe jijini Kampala Abiriga alijisaidia katika ukuta wa uzio wa wizara ya fedha kitendo ambacho ni kinyume cha sheria ya uendelezaji Mamlaka ya Jiji la Kampala ya mwaka 2016Facebook