Katibu Wa CHADEMA Kahama Ajivua Uanachama Na Kujiunga Na Ccm

KATIBU wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga amejivua uwanachama wa chama hicho na na nyadhifa zote alizokuwa nazo ndani ya chama na kujiunga Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akitangaza uamuzi huo Ndugu Michael Fabian Kigenda katika barua yake ya kujivua uwanachama na kuachia nafasi zake za uongozi ndani ya Chadema amesema haoni haja ya kuendelea kuwa mpinzani na kupingana na serikali ya Rais John Magufuli kwani Rais amekuwa akitekeleza agenda zote ambazo Chadema ilikuwa ikizihubiri na hivyo chama hicho kimekosa agenda kwa sasa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment