Manchester United Yaduwazwa Na leicester City

Klabu ya Manchester United jana Jumamosi usiku imeduwazwa kwa kulazimishwa sare ya goli 2-2 na klabu ya Leicester City waliocheza pungufu uwanjani, kwenye mchezo wa Ligi Kuu soka England.
Manchester United walionekana kuutawala mchezo huo kuanzia kipindi cha kwanza na ingawaje hadi mapumziko timu zote mbili zilikuwa zimeshafungana goli 1-1, magoli kutoka kwa Jamie Vardy na Juan Mata.
Kipindi cha pili United walianza kuuwasha moto na kufanikiwa kupata goli la pili kupitia kwa Mata kunako dakika ya 60 na watu wengi walijua mchezo ulikuwa umeisha baada ya beki wa Leicester City, Daniel Amartey kulimwa kadi nyekundu.
Leicester wakiwa pungufu walipambana mpaka dakika nne za nyongeza walipofanikiwa kusawazisha goli la pili na kuwaduwaza mashabiki wa Man United.
Kwa matokeo hayo Manchester United bado wamepunguzwa pointi katika mbio za kuusaka ubingwa wa EPL dhidi ya vinara wa Ligi hiyo, Manchester City. Tazama msimamo wa ligi hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment