Friday, June 26, 2015
Nkupamah blog
Mbunge
wa Babati Mjini (CCM), Kiseryi Chambiri, amesema anamuomba Mungu jina
la Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa liwe ni miongoni mwa majina
matatu ya wagombea urais yatakayofika katika Mkutano Mkuu wa CCM kwani
litakapoonekana watakuwa wamemaliza kazi na uchaguzi.
Kauli
hiyo aliitoa jana katika uwanja wa Old Majengo wilayani Babati wakati
wa kukabidhi wanachama wa CCM waliojitokeza kumdhamini Lowassa katika
mbio zake za kusaka urais kwa tiketi ya chama hicho. Katika Mkoa huo
alipata jumla ya wadhamini 42,405.
Chambiri
alisema safari ya Lowassa ni ndefu lakini karibu wanafika mwisho na
anachoomba katika majina matatu yatakayofika katika himaya yao kama
wajumbe wa Mkutano huo jina lake liwemo kusudi waweze kufanya kazi.
“Kwa
sababu kwa mujibu wa taratibu za CCM majina yale matatu huletwa ili
yaweze kupigiwa kura, kama jina lako halipo hatuwezi kufanya kazi na
mimi nakuombea kwa mungu basi katika yale majina matatu yatakayoletwa
kwaajili ya kupigiwa kura na lako liwepo,” alisema Chambiri.
Alisema endapo jina hilo litakuwapo watakuwa wamemaliza kazi na uchaguzi utakuwa umemalizika.
Naye
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha Onesmo Nangole, alisema matumaini
yaliyopo ni makubwa kwani Lowassa ni mtu mkarimu na mpole na chakula
chake huliwa na masikini na mtu mwenye nywele nyeupe anautukufu.
Akizungumza
na wanachama na wananchi, Lowassa aliwashukuru kwa kujitokeza
kumdhamini na kusema imani huzaa imani na kwamba atahakikisha akipata
nafasi hiyo atawatumikia.
“Nawashukuru
kwa wale walionidhamini najua CCM wanahitaji wachache lakini
nimedhaminiwa na wengi, nitaenda kuyahifadhi nyumbani kwangu kama
kumbukumbu na historia ya maisha yangu nasema nashukuru sana,” alisema Lowassa.
Aidha
alisema wakimchagua wahakikishe wanapenda kuchapa kazi maana anataka
kuendesha nchi mchakachaka ili kuondokana na umasikini.
Aliwawakumbusha
kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la
kupigia kura kwani ni haki yao ya msingi na kikatiba.
“Natamani niongee mengi lakini kanuni haziruhusi ibaki kusema naomba muendelee kuniombea katika hili na nina wapenda sana,” alisema Lowassa.
Awali
Katibu wa CCM Wilaya ya Babati, Daniel Ole Porokwa, alisema wanachama
wa CCM 42,405 wamejitokeza kumdhamini Lowassa katika mkoa huo tofauti na
wengine waliodai hatapata wadhamini wengi Manyara.
“Waliokudhamini
wote wamejitolea na ndiyo maana wapo hapa, haya ni mapenzi tu ya
wananchi na naamini wewe ndio utakayekuwa Rais wa Tanzania…Hakatwi mtu
hapa,”alisema.
Alisema
katika wilaya ya Mbulu wamemdhamini 9,500, Babati Mjini 12,500, Babati
Vijijini 6,000, Hanang' 5,700, Kiteto 5,550 na Simanjiro 10,300.
Nkupamah blog
0 comments :
Post a Comment