*Fanisi Venture Capital Fund imetoa dola za Kimarekani milioni 6 kwa maendeleo ya kampuni ya Kijenge Animal Product Limited.
Kijenge ni
kampuni mseto ya usindikaji iliyopo mkoani Arusha,ambayo inajihuhisha na
usagaji mahindi, uzalishaji wa chakula cha wanyama na kuku ambao wako
tayari kwa kula, kilimo na usindikaji. Kampuni hiyo iko katika mchakato
wa kujenga msingi kwa ajili ya awamu nyingine ya ukuaji ambapo kutakuwa
na ongezeko la vyanzo mbalimbali vya mapato yake kwa kuboresha
miundombinu yake ya sasa ya uzalishaji ikiwa ni pamoja na kuanzisha njia
mpya za uzalishaji.Fanisi itakuwa na jukumu kubwa la kuhakikisha
inasaidia ukuaji wa kampuni katika hatua ijayo na pia kutoa fedha za
mtaji kwa ajili kukuza hisa za Kijenge.
Akizungumzia
juu ya zoezi hilo, muasisi na mwenyekiti wa Kijenge, Andrew Mollel
amesema: “Baada ya mazungumzo binafsi ya miaka kadhaa ya kuhakikisha
hakuna anayepunjwa, tumeona kuwa Fanisi ni watu sahihi kwa maendeleo ya
Kijenge, na mtazamo wao ni zaidi ya msaada wa kifedha wanaotoa. Ubia huu
unatupa fursa ya kukuza mtaji wetu ambao utatusaidia kuboresha mbinu za
usambazi bidhaa zetu ili kukidhi mahitaji ya wateja kwa usahihi”.
Mkurugenzi
mwenza wa Fanisi Tony Wainanina amefurahiswa na mkataba huo pamoja na
ari kubwa ya kijasiriamali ambayo kampuni imefaidika ikiwa chini ya
uongozi wa Mollel. Wainanina amesema: “Tunaiunga mkono kampuni yenye
historia na jina kubwa katika soka la hapa nchini. Huu ndio mkataba wa
kwanza ambao tumefanikiwa kufikia makubaliano ambao tutakua tukiangazia
katika masula ya kilimo cha biashara hasa katika ukanda huu wa Afrika
Mashariki”.
Ujio huu wa
Kijenge umefanya Fanisi kuongeza wigo wake wa uwekezaji ambapo sasa ni
miongoni mwa makumpuni nane yaliyopo mkoani Arusha ambayo yanajuhisisha
na sekta mbalimbali ikiwemo za kilimo (hasa cha biashara), elimu, uuzaji
wa bidhaa za rejareja kwa wateja(FMCG) pamoja afya.
Sehemu
nyingine ambazo kampuni ya Fanisi imewekeza ni pamoja na Halton, duka la
dawa za rejareja ambalo linapatika zaidi ya sehemu 30 jijini Nairobi,
ambalo hivi karibuni limeingia ubia na Tuskys katika uhifadhi wa dawa
katika maeneo yao; Hillcrest International Schools, kundi la taasisi za
kielimu zenye mrengo wa mtaala wa Kiingereza; Prodev Group, Kampuni ya
usagaji na uuzaji mahindi iliyopo Rwanda; Sophar, duka la uuzaji na
usambaziaji dawa la jumla lililopo nchini Rwanda;Live Ad, kampuni
inayojiuhusha na matangazo ya nje iliyopo nchini Kenya na vilevile
European Foods Africa Ltd, kampuni inayojiuhusisha na utunzaji na
usambazaji wa vyakula ambayo kwa sasa inauza Piza, matunda na juisi
asilia.
Kampuni ya
Fanisi Capital ni kampuni ya uwekezaji miradi yenye thamani ya dola za
Kimarekani milioni 50, ambayo inalenga kuzizibadilisha sekta
mbalimbaliza kibiashara kama vile, Afya, Kilimo cha Biashara, Elimu na ,
Uuzaji wa bidhaa za rejareja kwa wateja.
Posted by Nkupamah blog
0 comments :
Post a Comment