Mufti Mkuu wa Tanzania 'Atumbua Majipu' Mengine.......Aivunja Mamlaka ya Usimamizi wa Msikiti Mkuu Arusha na Kuweka Mpya

  @nkupamah blog

Mufti mkuu wa Tanzania Sheikh Alhaji Abubakari Zuberi ameivunja mamlaka ya uendeshaji na usimamizi wa msikiti mkuu wa mkoa wa Arusha na kuweka mamlaka mpya ili kuimarisha utendaji.
 
Akitangaza maamuzi hayo kwa niaba ya mufti Sheikh mkuu wa mkoa wa Arusha Shabani Juma alisema anaamini kuwa mamlaka mpya iliyowekwa itafanya kazi kwa ufanisi na kwa kasi ya hali ya juu pamoja na kujipanua ili kwafikia waumini wengi kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwahudumia kwa ukaribu.

Hata hivyo baadhi ya wajumbe wa mamlaka iliyovunjwa wamesema kuwa hawajaridhishwa na uamuzi huo kwani hawakushirikishwa wakati wa vikao vya maamuzi vya mkoa vilivyojadili majina kumi na tano ya wajumbe yaliyotumwa kwa mufti kwa ajili ya uteuzi huo wa mamlaka mpya.

Kwa upande wao wajumbe wapya waliochaguliwa kuingia katika mamlaka hiyo mpya wamesema kuwa wanachangamoto kubwa ya kuwaunganisha waumini pamoja na viongozi wao ili kuleta maendeleo na kudumisha mshikamano.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment