Ligi Kuu ya Uingereza jana usiku iliendelea kwa michezo mitano.
Chelsea iliwafata Norwich katika uwanja wa Carrow Road na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja, magoli ya Chelsea yalifungwa na Robert Kenedy katika dakika ya kwanza ya mchezo huo na goli la pili likifungwa na Diego Costa dakika ya 45.
Goli la Norwich lilifungwa na Nathan Redmond dakika ya 68 na hadi mwamuzi Lee Mason anamaliza mchezo huo Chelsea ilikuwa mbele kwa goli mbili kwa moja.

Mchezo mwingine ni vinara wa ligi hiyo, Leicester City walitoka sare ya goli  2 – 2  na West Bromwich Albion.
Matokeo mengine ni;
Bournemouth 2 – 0 Southampton
Aston Villa 1 – 3 Everton
Sunderland 2 – 2 Crystal Palace