Maafisa wa Jeshi la Mageereza
wakiwa wameubeba mwili wa Marehemu Mkaguzi wa Magereza, Morice Peter
wakiuingiza nyumbani kwake kabla ya kutoa heshima za
mwisho leo Desemba
24, 2015 katika Viwanja vya Gereza Kuu Ukonga Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Marehemu Mkaguzi wa
Magereza, Morice Peter(vazi jeupe) akiwa kwenye majonzi makubwa wakati
wa kuaga mwili wa mwenzi wake. Marehemu ameagwa leo katika Viwanja vya
Gereza Kuu Ukonga Jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwa mazishi
nyumbani kwao Mkoani Morogoro.
Mkaguzi wa Magereza, Seleman Sued
wa Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam akisoma Wasifu wa Mkaguzi wa
Magereza Morice Peter aliyefariki juzi Desemba, 2015 katika Hospitali ya
Dar Group, Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Magereza waliohudhuria katika hafla ya kuaga mwili wa Marehemu Mkaguzi wa Magereza, Morice Peter.
Mke wa Marehemu Mkaguzi wa
Magereza, Dorice Peter(kulia) akipewa msaada ndugu wa karibu wakati wa
kusindikiza mwili kuelekea kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea
Mkoani Morogoro kwenye mazishi.
Ndugu na jamaa waliojitokeza
kuuaga mwili wa Marehemu Mkaguzi wa Jeshi la Magereza, Morice Peter
aliyekuwa akihudumu katika Gereza Kuu Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi Morice Peter amefariki juzi Desemba 22, 2015 baada ya kuugua
muda mrefu katika Hospitali ya Dar Group Jijini Dar es salaam.
0 comments :
Post a Comment