DAR ES SALAAM
Serikali imeitangaza rasmi siku ya
jumamosi ya kila mwisho wa mwezi kuwa ni siku ya usafi na kwamba hatua
za kisheria na kinidhamu zitachukuliwa kwa watendaji wowote
watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo.
Agizo hilo limetolewa jijini Dar es
Salaam na naibu waziri wa ofisi ya makamo wa rais, muungano na mazingira
Bw Luoga Mpina ambapo amesema agizo hilo linaanza mara moja huku
akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kupambana na magonjwa yanaweza
kusababishwa na uchafu.
Kuhusu athari za mabadiliko ya tabia
nchi waziri Mpina amesema Tanzania hupoteza zaidi ya heka laki nne za
misitu kila mwaka huku joto la dunia likiongeza kwa nyuzi joto 0.85,
ambapo pia kina cha bahari kikiongeka hadi kufikia 19 cm, pia akatumia
fursa hiyo kutoa agizo kwa halimashauri zote nchini.
Kwa mujibu wa taarifa za wizara hiyo
ya makamo wa rais muungano na mazingira, Tanzania inazaidi ya hekta
milioni 48.1 za misitu ambayo hutumika kumeza hewa ya kabon tirion 9.03
ambapo juhudi za upandaji miti zikitajwa kusaidia kuondoa athari za
mabadiliko ya tabia nchi.
0 comments :
Post a Comment