ONGEZENI IDADI YA WATUMIAJI MAJI DAR – PROF MBARAWA

    @nkupamah blog
    Mh. Prof. Mbarawa akiongea na menejimenti ya Dawasco na Dawassa kwenye ukumbi wa Dawasco gerezani,mwishoni mwa wiki jijini Dar.(picha na @nkupamah blog
    Mh. Prof. Makame Mbarawa akisaini kitabu cha wageni akiwa na Naibu waziri,Injinia Isack Kamwelwe (kushoto), pamoja na katibu mkuu na naibu katibu mkuu wa wizara ya maji (kulia) katika ofisi ya afisa mtendaji mkuu wa Dawasco.
    Waziri wa maji mh. Prof. Makame Mbarawa akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Dawasco mapema leo alipotembelea makao makuu ya ofisi hizo
    Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Injinia Cyprian Luhemeja akiwa na waziri wa maji Prof. Makame Mbarawa mara tu baada ya kuwasili katika ofisi hizo

    Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (Dawasco) limetakiwa kuongeza idadi ya wananchi wanaopata Maji jijini Dar es salaam kutoka wateja 148,000 waliopo sasa hadi wateja milioni 1 ifikapo Juni 2016.(VICTOR)
    Akiongea na Menejimenti ya Dawasco na Dawasa ikiwa ni siku moja tangu kuchaguliwa kwake Waziri wa Maji Mh. Prof Makame Mbarawa alizitaka Taasisi hizo kuweka mkakati wa lazima utakao hakikisha wateja milioni wanaunganishwa kwenye mtandao wa Majisafi na salama kwa wakazi wote jijini.Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Injinia Cyprian Luhemeja akiwa na waziri wa maji Prof. Makame Mbarawa mara tu baada ya kuwasili katika ofisi hizo Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (Dawasco) limetakiwa kuongeza idadi ya wananchi wanaopata Maji jijini Dar es salaam kutoka wateja 148,000 waliopo sasa hadi wateja milioni 1 ifikapo Juni 2016.
    Akiongea na Menejimenti ya Dawasco na Dawasa ikiwa ni siku moja tangu kuchaguliwa kwake Waziri wa Maji Mh. Prof Makame Mbarawa alizitaka Taasisi hizo kuweka mkakati wa lazima utakao hakikisha wateja milioni wanaunganishwa kwenye mtandao wa Majisafi na salama kwa wakazi wote jijini.
    “Tumekuja kutekeleza ahadi ya Rais Magufuli aliyoitoa bungeni kuhusu Maji. Aliahidi Serikali ya awamu ya tano pamoja na mambo mengine watahakikisha wana mtua Mama ndoo kichwani” alisema Mh Waziri.
    Aliongeza kuwa lazima taasisi hizi mbili zijue wajibu wake kwa wananchi na kutekeleza ahadi ya Rais ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa kutafuta Maji na hata wakiyapata gharama zisiwe juu, ameitaka Dawasco kuhakikisha inawahimiza wateja wake wote na taasisi za serikali kulipia Ankara za Maji kwa wakati.
    Aidha amewahimiza Dawasa kuboresha mtandao wa Majitaka ili kuwafikia wateja wengi zaidi wanaohitaji huduma hiyo ya Majitaka na kuepusha usumbufu kwa wananchi unaotokana na Majitaka hayo kuendelea kumwagika ovyo katika mitaa mingi ya jiji.“Hakikisheni mnaboresha mfumo wote wa Majitaka, uendane na mahitaji ya sasa ya jiji ili kuwapunguzia wananchi kupata kero mbalimbali zinazotokana na uchavu wa miundombinu ya Majitaka” alisema Mh.Mbarawa.
    “Tumekuja kutekeleza ahadi ya Rais Magufuli aliyoitoa bungeni kuhusu Maji. Aliahidi Serikali ya awamu ya tano pamoja na mambo mengine watahakikisha wana mtua Mama ndoo kichwani” alisema Mh Waziri.
    Aliongeza kuwa lazima taasisi hizi mbili zijue wajibu wake kwa wananchi na kutekeleza ahadi ya Rais ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa kutafuta Maji na hata wakiyapata gharama zisiwe juu, ameitaka Dawasco kuhakikisha inawahimiza wateja wake wote na taasisi za serikali kulipia Ankara za Maji kwa wakati.
    Aidha amewahimiza Dawasa kuboresha mtandao wa Majitaka ili kuwafikia wateja wengi zaidi wanaohitaji huduma hiyo ya Majitaka na kuepusha usumbufu kwa wananchi unaotokana na Majitaka hayo kuendelea kumwagika ovyo katika mitaa mingi ya jiji.“Hakikisheni mnaboresha mfumo wote wa Majitaka, uendane na mahitaji ya sasa ya jiji ili kuwapunguzia wananchi kupata kero mbalimbali zinazotokana na uchavu wa miundombinu ya Majitaka” alisema Mh.Mbarawa.
    Share on Google Plus

    About Unknown

    This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
      Blogger Comment
      Facebook Comment

    0 comments :

    Post a Comment