WANANCHI WATAKIWA KUFANYA ZOEZI LA USAFI ENDELEVU WILAYANI TEMEKE

TM1 
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(katikati)  akitoa mwongozo jana juu ya suala la kufanya usafi kwa wakuu wa idara(hawapo pichani) wa Halmashauri wa Manispaa ya Temeke. Wengine katika picha ni Mkurugezi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo (kushoto) na Mkurugenzi wa  Utumishi na Raslimali Watu wa TAMISEMI Bw. Mohamed Pawaga(kulia)
TM2 
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba akisisitiza juu ya utekelezaji wa agizo la Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  la usafi wa mazingira ,jana wakati alipotembelea Ofisi ya Msimamizi wa soko la Temeke Sterio lililopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
TM3Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(aliyetangulia) akikagua machinjio ya kuku jana katika soko la Temeke Sterio Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
TM5 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo (wa pili kushoto) akimwongoza  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(katikati)  kukagua soko la Temeke Sterio lililopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.Zoezi hilo lilifanyika jana wilayani humo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  la usafishaji wa mazingira.
TM6Katapila la Halmashauri la Manispaa ya Temeke likizoa uchafu jana katika soko la Temeke Sterio ikiwa ni utekelezaji agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  la usafishaji wa mazingira.
TM7Takataka zikiwa zimezagaa mitaani baada ya kutupwa na wananchi wa Kiburugwa katika Manispaa ya Temeke.
TM9Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(kulia)  akitoa agizo kwa  Mkuu wa Idara ya Usafishaji na Manispaa ya Manispaa ya Temeke Bw. Ally Hatibu ya kuondoa mara moja uchafu katika eneo la barabara ya Kiburugwa ambayo wakazi wa huko wamegeuza sehemu ya kutupa takataka.  Agizo hilo alilitoa jana wakati alipofanya ziara ya kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  la usafishaji wa mazingira.
 Picha zote na Beatrice Lyimo -MAELEZO
………………………………………………………………………………………..
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
 
Dar es salaam
 
Serikali imewataka wananchi wote kuwajibika katika usafishaji wa mazingira na maeneo yanayowazunguka ili kudhibiti magonjwa mbalimbali ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.
Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Zuberi Samataba wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ya ukaguzi na utoaji mwongozo katika kutekeleza agizo la Rais la kutumia siku ya Uhuru kufanya usafi.
Alisema kuwa kila mwanachi anapaswa kuhakikisha mazingira anayoishi na yale yanayomzunguka yanakuwa safi wakati wote ili kupunguza mlipuko wa kipindupindu.
Samataba alisema kuwa mazingira yanayowazunguka wananchi yakiwa safi yatapunguza matumizi ya serikali yanatokana na ununuzi wa dawa za kutibu wagonjwa wa kipindupindu na hivyo fedha hizo kuelekezwa katika matumizi mengine.
“Kila mmoja akiwajibika mahali pa kazi na mazingira yanayomzunguka hali hii itasaidia kuimarishwa usafi na hivyo kila mtu anapaswa awajibike kwa uchafu anaouzalisha nyumbani kwake au sehemu ya kazi yake kwani jukumu la usafi ni la kila mtu” alisisitiza . Samataba.
Alisema kuwa kila Halmashauri nchini inapaswa kujipanga vizuri katika kuhakikisha kuwa inaondoa uchafu mitaani na kusafisha maeneo yake  ili kuondokana na tatizo la kipindupindu.
Samataba aliwaagiza viongozi wa Manispaa ya Temeke na Halmashauri nyingine nchini kusimamia suala la usafi  kuhakikisha linakuwa  endelevu kwani jukumu la usimamizi wa usafi ni la kila mtu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Photidas Kagimbo alisema kuwa wananchi wa Halamashauri hiyo wamelipokea suala la utekelezaji wa agizo la Rais na wanaahidi kuhakikisha kuwa maeneo yote yanakuwa safi siku zote.
 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment