@nkupamah blog
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Charles Kitwanga (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo,
Mbarak Abdulwakil (kulia) na Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo mara baada
ya kumpongeza Waziri huyo mpya, nje ya Ukumbi wa Mikutano Ikulu, jijini
Dar es Salaam. Picha na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kushoto) akimkaribisha Waziri mpya wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, ndani ya ofisi ya
waziri huyo
iliyopo Mtaa wa Ohio, jijini Dar es Salaam. Picha na Felix Mwagara,
Kitengo cha Mawasiliano-MOHA
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Charles Kitwanga akisaini kitabu cha wageni kilichopo ndani ya ofisi
yake, mara baada ya Waziri huyo mpya kuingia ndani ya ofisi hiyo baada
ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Picha na Felix Mwagara,
Kitengo cha Mawasiliano-MOHA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wapili kushoto) akimfafanulia Waziri
mpya wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga (kulia), shughuli mbalimbali
zinazofanywa na wizara hiyo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo.
Tukio hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo jijini
Dar es Salaam, mara baada ya Waziri huyo kuapishwa Ikulu leo. Picha na
Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Charles Kitwanga (kulia) akijadiliana na watendaji wa wizara hiyo kuhusu
masuala mbalimbali ya wizara hiyo, mara baada ya Waziri huyo kuapishwa
Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Wanne kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara
hiyo, Mbarak Abdulwakil, anayefuata ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo,
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP), John Minja, Naibu Mkuu wa
Jeshi la Polisi (D/IGP), Abdurahman Kaniki na Kamishina wa Fedha na
Utawala wa Idara ya Uhamiaji, Piniel Mgonja (hayupo pichani). Picha zote
na Felix Mwagara, Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.


0 comments :
Post a Comment