uhitaji zikiwemo Zahanati ,vituo vya afya,ofisi za watendaji kata na
shule mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia kuboresha huduma zao
wanazotoa kwa jamii. Hayo yalisemwa jana na Meneja masoko wa kampuni ya Sola ya Mobisol
,Seth Matemu na Meneja Mauzo ,Joseph Zikhali wakati wakizungumza na
waandishi wa habari katika hafla ya kutangaza ofa mpya ya msimu wa
sikukuu kwa wateja wake .
Alisema kuwa, kampuni hiyo ya sola imekuwa ikisaidia shughuli
mbalimbali za kijamii hususani zenye uhitaji ambapo hadi sasa hivi
wamekwisha tumia kiasi cha shs 15 milioni kwa ajili ya kusaidia
mitambo hiyo .
Matemu alisema kuwa, lengo la kuwasaidia jamii hiyo ni mojawapo ya
malengo ya kampuni hiyo kuhakikisha kuwa inarudisha sehemu ya faida
kwa wananchi wake kwa kugawa mitambo ya sola bure kwa wenye mahitaji.
Alisema kuwa,kampuni hiyo ina zaidi ya wateja 20,000 kwa Tanzania
nzima ambapo wananchi wengi kwa sasa wana mahitaji ya umeme wa jua
kutokana na changamoto kubwa ya umeme unaokatika kila wakati na hivyo
kuchangia baadhi ya shughuli kusimama .
Naye Meneja wa huduma kwa wateja kutoka kampuni hiyo, Tery Odiko
alisema kuwa, kampuni hiyo imejiwekea mikakati zaidi ya kuhakikisha
inafikisha huduma zake katika maeneo ya vijijini ambapo huduma za
umeme hazijawafikia wananchi.
Alisema kuwa,huduma hizo wanazotoa zimekuwa zikisaidia kukuza ajira
kwa vijana kwani kwa kumiliki mitambo hiyo wana uwezo wa kuanzisha
shughuli mbalimbali za kuwaingia kipato muda wote kama vile salon
sehemu ya kuchajia simu kwa kuwa na umeme wa uhakika.
Aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kununua mitambo ya sola kwa
msimu huu wa sikukuu kwani wanatoa ofa maalumu kwa wateja wake
0 comments :
Post a Comment