Familia nchini Uchina sasa zimeruhusiwa kupata watoto wawili baada ya kuanza kutekelezwa kwa sera mpya kuhusu upangaji
uzazi.
Sera
hiyo mpya imeanza kutekelezwa Ijumaa na kufikisha kikomo sera tata ya
awali ambayo iliwaruhusu wanandoa kupata mtoto mmoja pekee.
Sera hiyo imesababisha kuwepo kwa sehemu kubwa ya raia ambao ni wazee na kupungua kwa watu ambao wanaweza kufanya kazi.
Sera hiyo ya watoto waili ilitangazwa Oktoba na chama tawala cha Kikomunisti na kuidhinishwa na bunge la taifa baadaye Desemba.
"Ni vyema kuzingatia jinsi maisha yataathirika,” shirika la habari la serikali la Xinhua limesema.
Sera ya kuruhusu mtoto mmoja pekee katika familia ilianza kutekelezwa mwaka 1978.
Waliopata watoto zaidi waliadhibiwa vikali na hata wengine kulazimishwa kutoa mimba.
Sera hiyo ilizuia kuzaliwa kwa watoto zaidi ya mmoja.
Idadi ya watu Uchina kufikia 2013 wakati wa kufanywa kwa sensa ilikuwa imefikia 1.357 bilioni.
Kufikia 2050, Uchina inatarajiwa kuwa na watu karibu 500 milioni waliozidi umri wa miaka 60, idadi inayozidi raia wa Marekani.
Utafiti
uliofanywa majuzi unaonyesha kwamba licha ya serikali kulegeza sheria
ya kujifungua watoto, hakuna msisimko miongoni mwa wanandoa 100 milioni
ambao wanaweza kupata watoto wa ziada.
Hii sana inatokana na gharama ya kuwalea watoto.
0 comments :
Post a Comment