Hali ya Mufti Mkuu Abubakar Zuberi Yaimarika Baada Ya Kufanyiwa Upasuaji Wa Tumbo

Nkupamah Media:


Hali ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu wa Tanzania Abubakar Zuberi ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu inaendelea vizuri.

Ofisa Uhusiano wa MNH, Neema Mwangomo jana alisema mufti amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete   na alifikishwa  Hospitalini  hapo  juzi. 

Jana, viongozi  mbalimbali  wa  serikali  akiwemo  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa walimtembelea  kumjulia hali  Mufti Zeburi

Pia,baadhi ya waumini wa Kiislamu jana mchana walionekana nje ya jengo hilo wakitaka kufahamu maendeleo ya afya ya kiongozi wao huyo. 

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment