JESHI LA POLISI LIMEJIPANGA KUIMARISHA ULINZI WAKATI WA UPIGAJI KURA KWENYE UCHAGUZI WA MARUDIO ZANZIMBAR.

Nkupamah media










Kamishna wa Jeshi la  Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame amesema kwamba Jeshi hilo limejipanga kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya Unguja na Pemba wakati wa upigaji kura kwenye uchaguzi wa marudio .
 Akizungumza na gazeti hili Kisiwani Pemba Kamishna Hamdan amewatoa hofu  wananchi kuwa hakuna  mwananchi  mwenye sifa ya kupiga kura ambaye hataweza kwenda kupiga kura tarehe 20 machi mwaka huu wakati wa uchaguzi wa marudio  kutokana na sababu za vitisho .
Amesema kwamba tayari Jeshi la Polisi limeanza kutengeneza mazingira ambayo yatawaweza wananchi kila mmoja kuwa huru na kuhakikisha kuwa usalama wa nchi utaendelea kudumishwa .
Katika mazungumzo na gazaeti hili katika Makao Makuu wa Jeshi hilo Mkoa wa Kaskazini Pemba , Kamishna Hamdan amefahamisha hakuna mwananchi ambaye hatapiga kura kutokana na vitisho , labda aache kwa sababu zake mwenyewe .
“Hakuna mwananchi ambaye atapata fursa ya kupiga kura kwa sababu za vitisho , labda yeye asiende kwa sababu anazozijua yeye , lakini sio suala la vitisho ulinzi utaimarishwa maeneo yote ya Unguja na Pemba ”alisisitiza Hamdan .
Aidha Kamishna Hamdan amesema pamoja na kazi ya ulinzi wa wananchi na mali zao  kuwa ni Polisi , lakini iko haja kwa wananchi nao kuwapa ushirikiano askari pindi wanapobaini kuwa viasharia vya vitisho au uvunjifu wa amani .
Ameeleza kwamba ni kazi ya Jeshi la Polisi kuona  wanannchi wanaishi kwa amani katika nchi yao na wanafanya mambo kwa mujibu wa sheria , na kuongeza tayari changamoto zinazojitokeza ikiwemo vitisho wanazifahamu na wanazifanyia kazi ili zisilete athari wakati wa zoezi la uchaguzi .
“Niwahakikishie wananchi kwamba changamoto  zinazojitokeza ikiwemo vitisho tunazifahamu  , na tunashukuru wanazisema wazi wazi , labda niwahakikishie wananchi tumejipanga kuzikabili ili zisileta madhara  kabla na baada ya uchaguzi huo ”alifahamisha .
Kamishna Hamdan  pia ameeleza  kwamba Jeshi limejipanga pia kubadilisha mfumo wa kusimamia ili changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi uliofanyika 25, oktoba mwaka jana wazigeuze kuwa fursa .
Akizungumza ulinzi katika maeneo ya Visiwa Vidogo vidogo , amesema kwamba watawatumia askari shehia kutoa taarifa ili waweze kuyafikia maeneo yote huku akisisitiza kwamba namba za simu za makanda wa Polisi Mikoa yote ziko wazi na zinafahamika na wananchi waliowengi .
“Sisi tupo wengi na maeneo yote tunayafahamu , kwa hili tutawatumia zaidi askari wetu wa shehia na kikubwa zaidi ni kwamba makamanda wote wa mikoa Zanzibar namba zao za simu ziko wazi muda wote wananchi wanatakiwa kuwapigia na kuwaeleza changamoto zinazowakabili ”alieleza.
Hata hivyo alisema kwamba Jeshi la Polisi litafanya kazi kwa karibu na Serikali za  Shehia kwa kuwatumia masheha na kamati zao kuhakikisha taarifa zote za uvunjifu wa amani zinaripotia na zinachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria .
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment