Aidha, amepiga marufuku wanaume kupokea fedha hizo kwa niaba ya familia zao akisema wengi si
waaminifu linapokuja suala la fedha.
Alitoa maagizo hayo mjini hapa alipokuwa akizungumza na madiwani, wakuu wa idara na viongozi wa vyama vya siasa wilaya ya Songea katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini.
Alisisitiza wanaume kutopewa fedha akisema utafiti unaonesha wengi wao si watunzaji wazuri wa fedha na tayari malalamiko yameibuka, baadhi ya wanaume wakituhumiwa kunywea pombe na wengine kuongeza idadi ya wanawake.
“Waheshimiwa madiwani nawaomba sana nendeni mkasimamie utekelezaji wa jambo hili, fedha hizi zikitunzwa na wanawake hakika zinakuwa salama zaidi kuliko zikitunzwa na sisi wanaume,” alisema Mwambungu.
Alisema akinamama wengi ni waaminifu sana ikilinganishwa na wanaume hivyo ni vizuri wanaopaswa kupokea malipo ya fedha hizo za ruzuku kwa ajili ya kuwezesha kaya masikini na familia zinazoishi katika mazingira magumu ni wanawake na siyo wanaume ambao kila siku wamekuwa mabingwa wa kuzalisha vitendo viovu ambavyo vinachangia kusambaratisha familia.


0 comments :
Post a Comment