RC azuia wanaume kupokea fedha Tasaf


MKUU wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu, amewaagiza watendaji wa vijiji, mtaa na kata katika mkoa huo kuwachukulia hatua wanaume wanaotumia fedha zinazotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf III) kunywea pombe, badala ya malengo yaliyokusudiwa ya kuziinua kiuchumi familia zao.
Aidha, amepiga marufuku wanaume kupokea fedha hizo kwa niaba ya familia zao akisema wengi si
waaminifu linapokuja suala la fedha.
Alitoa maagizo hayo mjini hapa alipokuwa akizungumza na madiwani, wakuu wa idara na viongozi wa vyama vya siasa wilaya ya Songea katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini.
Alisisitiza wanaume kutopewa fedha akisema utafiti unaonesha wengi wao si watunzaji wazuri wa fedha na tayari malalamiko yameibuka, baadhi ya wanaume wakituhumiwa kunywea pombe na wengine kuongeza idadi ya wanawake.
“Waheshimiwa madiwani nawaomba sana nendeni mkasimamie utekelezaji wa jambo hili, fedha hizi zikitunzwa na wanawake hakika zinakuwa salama zaidi kuliko zikitunzwa na sisi wanaume,” alisema Mwambungu.
Alisema akinamama wengi ni waaminifu sana ikilinganishwa na wanaume hivyo ni vizuri wanaopaswa kupokea malipo ya fedha hizo za ruzuku kwa ajili ya kuwezesha kaya masikini na familia zinazoishi katika mazingira magumu ni wanawake na siyo wanaume ambao kila siku wamekuwa mabingwa wa kuzalisha vitendo viovu ambavyo vinachangia kusambaratisha familia.
Share on Google Plus

About Mng'atuzi blog

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment