Staa Diamond Platnumz
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG.
Staa
wa muziki nchini Naseeb Abdul Juma a.k.a Diamond Platnumz ametakiwa
kutoka Jijini Dar es salaam na kurejea Mkoani Kigoma alikozaliwa, ili
kuwasaidia Wasanii chipukizi katika Mkoa huo.
Mbali
na Diamond, Staa mwingine alietajwa ili atoke Jijini Dar es salaam na
Kurejea Mkoani kwake ni Farid Kubanda a.k.a Fid Q, ambae ametakiwa
kurejea Jijini Mwanza ili kusaidia kuukuza muziki wa Mwanza
Mbali
hao mastaa hao ambao wametajwa live majina yao, pia mastaa wote
waliohamishia shughuli zao za sanaa Jijini Dar es salaam wametakiwa
kurejea katika Mikoa yao ili kuondoa mrundikano wa wasanii katika Jiji
hilo.
Hayo
yalisemwa juzi ijumaa Jijini Mwanza na Msanii Chipukizi Joseph Stanford
a.k.a Rich4D, katika hafla ya kumpongeza kwa ushujaa wake wa kutembea
kwa miguu kutoka Jijini Mwanza hadi Jijini Dar es salaam, kwa ajili ya
Kumpongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kutambua mchango wa wasanii
nchini na kuwajumuisha katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo.
“Wasanii
wakubwa watoke Jijini Dar na warudi Mikoani kwao ili wawasaidie wasanii
chipukizi wa Mikoani. Diamond arudi Kigoma. Fid Q arudi Mwanza. Hii
itaondoa mrundikano wa wasanii wakubwa Dar na hivyo kupeleka fursa za
sanaa mikoani”. Alisema Rich4D.
Matembezi
ya Miguu ya Msanii Rich4D yalianza Januari 16,2016 yakihusisha mikoa
minane sawa na Kilomita 1,200 na yalifikia tamati Februari 10,2016,
lakini adhma yake ya kuonana na rais haikuweza kutimia baada ya rais
kuwa katika majukumu mengine ya kitaifa ambapo aliekuwa Katibu Mkuu
Ombeni Sefue aliahidi msanii huyo kuonana na rais.
Wadau
mbalimbali waliosaidia kufanikisha matembezi hayo akiwemo Mwenyekiti wa
CCM Wilaya ya Nyamagana Raphael Shilatu pamoja na Mbunge wa Jimbo la
Nyamagana Stanslaus Mabula, wameyapongeza matembezi hayo na kusema kuwa
ni ya kizalendo ambapo wamemuomba Katibu Mkuu Mpya, Mhandisi John Kijazi
kuhakikisha ahadi aliyoiacha Sefue inatimia ili msanii Rich4D afanikiwe
kuonana na rais magufuli.
Staa Fid Q
Msanii Rich4D anaechipukia kwa kasi Jijini Mwanza ambapo tayari anatamba na ngoma mbili ambazo ni “Tawile” na “Huniwezi”.
Kutazama ilivyokuwa BONYEZA HAPA.




0 comments :
Post a Comment