Bunge Sports Club na Baraza la Wawakilishi hakuna mbabe, zatoka sare ya bao 1-1 uwanja wa Amani Zanzibar

Timu ya Mpira wa miguu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano la Tanzania,  Bunge Sports Club  usiku wa leo Aprili 26.2016 imeweza kutoka sare ya bao 1-1, dhidi ya timu ya Baraza la Wawakilishi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, mchezo uliochezwa uwanja wa Amaan, Unguja na kushuhudiwa na watu mbalimbali.
Mchezo huo wa aina yake na wa kipekee kwa  kikosi hicho cha  Bunge Sports Club kiliweza kucheza kandanda safi na la kuvutia wakati wote ambapo waliweza kupata bao lao la kuongoza  ndani ya dakika 22 ya mchezo katika kipindi cha kwanza bao safi lililofungwa kwa kushuti la nje ya 18 na kuwaacha Wachezaji wa Baraza la Wawakilishi wasijue la kufanya.
Bao hilo la Bunge Sports Club ambalo lilikuwa la ushindi lilidumu hadi  kipindi cha pili ambapo katika dakika ya 67, Timu  ya Baraza la Wawakilishi ilifanikiwa kusawazisha bao hilo na kufanya mchezo kuwa 1-1. Bao hilo lilipachikwa kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya hasa mvua kiasi cha kuwapoteza vibaya wachezaji wa timu ya Bunge ambao walicheza katika mazingira magumu sana.
Mara baada ya mchezo huo kumalizika, Kocha wa timu hiyo ambaye pia Mbunge Jimbo la Kilolo mkoani Iringa, Mh. Venance Mwamoto alibainisha kuwa kikosi chake kilicheza soka safi na wataendelea kukiimalisha kwani wanaamini mpira ni ajira ambapo pia alieleza kuwa bila washindani wao ‘kuwachomekea’ wanahakika wangefanya vizuri zaidi n ahata kuibuka na mabao mengi.
Kwa upande wake, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid alizipongeza timu zote mbili na kuzitaka kuendelea kudumisha michezo na suala la Muungano kwa ujumla kwani wanahakika kupitia michezo suala hilo litaenziwa kwa miaka yote.
Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu Wa Rais  Mazingira na Muungano Mh. January Makamba alibainisha kuwa wataendelea kuulinda Muungano huku akiwataka Watanzania kuishi kwa misingi ya Amani na utulivu kwa kipindi chote ambapo pia alieleza kuwa suala la Michezo litaendelea kuwapo ilikuongeza mshikamano kwa watu wote.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment