MAAFISA HABARI MKOA WA MWANZA WANUFAIKA NA VITENDEA KAZI KUTOKA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO


15 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella (aliyesimama) akizungumza na wadau wa sekta za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Mhe. Nape Nnauye kukutana na wadau hao jana Jijini Mwanza pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo jijini hapo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Baraka Konisaga na kulia ni katibu wa CCM Mwanza Ndg. Miraji Mtaturu
14 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella (wapili kulia) akizungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye alipowasili ofisini kwake wakati wa ziara yake jana Jijini Mwanza kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa na kutembelea viwanja vya Michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo Jijini Mwanza. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Baraka Konisaga na kulia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Ndaro Kulwijira.
16 
Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza Ndg. Atley Kuni akitoa taarifa ya sekta ya habari kwa mkoa wa Mwanza wakati wa ziara ya Mhe. Nape Nnauye kukutana na wadau wa sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo jana Jijini Mwanza pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo jijini hapo.
17 
Msanii kutoka jiji la Mwanza Ndg. Feizal Saul (aliyesimama) akichangia wakati wa ziara ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji jana Jijini Mwanza
18 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akimkabidhi iPad afisa habari kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Bw. Stephen Msengi wakati wa ziara ya yake kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia jana Jijini Mwanza pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo jijini hapo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella
19 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akimsikiliza Meneja wa Star times kanda ya ziwa Bw. Bakari Hassani (kushoto) alipotembelea ofisi hizo wakati wa ziara yake kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia jana Jijini Mwanza pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo jijini hapo.
20Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na watendaji wa TBC pamoja na Star Times nje ya ofisi za TBC zilizopo jijini Mwanza jana wakati wa ziara yake kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo jijini hapo. Wapili kushoto ni Meneja wa Star times kanda ya ziwa Bw. Bakari Hassani na watatu kulia ni Kaimu Mkuu wa Kanda ya ziwa TBC Bibi. Rachel Mwasha.
21 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akisalimiana na viongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza alipowasili katika uwanja vya CCM Kirumba kupata taarifa ya uwanja huo wakati wa ziara yake kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo na kutembelea viwanja vya michezo na vituo vya utangazaji vilivyopo Jijini Mwanza. Kushoto ni Katibu wa CCM Mwanza Ndg. Miraj Mtaturu.
Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo, Mwanza
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment