Kwa
kipindi cha karne hii ya 21, vijana wenye umri wa chini wamekuwa
watumwa wa mitandao ya kijamii, je nini hasara na faida zake?
Kumekuwa
na kesi nyingi zinazoendelea kuhusu Internet Addiction Disorder( IAD),
ambapo umekuwa ni ugonjwa unaokufanya usiweze kukaa au kufanya kitu
bila kupitia kwenye internet, hali hii imesadikika kuweza kuangamiza
kizazi kikubwa cha karne ya 21, na hasa kuleta matatizo katika mishipa
ya fahamu, matatio ya kisaikolojia na ya kijamii.
Matatizo
ya mishipa ya fahamu yanapelekea hata kuwa na uwezo mdogo wa kufikiria
kwa haraka hasa pale unapokuwa upo makini katika kuperuzi simu yako, pia
kichwa kuuma kwa muda mrefu kwa kutumia muda mwingi katika simu yako
na hata baadae kuchoka kiakili na kushindwa kufanya shughuli za
kimaendeleo .
Kisaikolojia
inamuharibu kijana hasa katika uwezo wa kufikiri na kuwaza, anaweza
kujihisi hawezi kukaa bila simu yake, hawezi kukaa bila kujua nani
kafanya nini au afanye nini kuwaridhisha marafiki wa kurasa za facebook
na Instagram, na hata kupelekea kuleta matabaka katika jamii watu
kujuana kiundani na kutengeneza chuki kwa baadhi ya watu au nchi, na
hata kuleta kuigana katika mtindo wa maisha.
Watu
wengi wamelalamika kuhusiana na kuaibishwa kupitia mitandao ya kijamii,
lakini kwa baadhi ya nchi kama Tanzania kumekuwa na sheria za kuzuia
matumizi mabaya ya internet.
Lakini pia, kwa upande wake Andrea Guzzoni ambaye ni Meneja Mkazi wa kampuni ya JovagoTanzania alifafanua kuwa, Matumizi ya tovuti yanafaida kubwa kiuchumi, watanzania hawana budi kuangalia suala hili kwa upande wa pili.
“Tutumie
kurasa za facebok, Instagram na Twitter katika kujifunza mambo ya
kimaendeleo na kutangaza biashara zetu, lakini pia serikali inabidi
iwajibike katika kuzuia baishara za utapeli zinazoendelea ndani ya
mitandao” aliongezea.
“Wapo
waliofanikiwa kupitia hii mitandao na wapo wanaondelea kuharibikiwa
kupitia mitandao hiyo hiyo, ni wakatai wa kubadilika na kutumia uhuru wa
habari kwa manufaa yetu”. Lilian Kisasa, Meneja Mawasiliano wa Jovago Tanzania aliongezea.
0 comments :
Post a Comment