Ligi
Kuu ya Uingereza usiku wa Jumatatu iliendelea kwa mchezo mmoja kati ya
Tottenham na West Brom Albion ambapo ulimalizika kwa sare ya goli moja
kwa moja.
Totttenham
ilikuwa ya kwanza kupata goli baada ya beki wa West Brom, Graig Dawson
kujifunga dakika ya 33 na baadae dakika ya 73 kusawazisha makosa na
kuisawazishia West Brom goli na hadi dakika ya 90 wakatoka moja kwa
moja.
Baada
ya matokeo hayo, tofauti ya alama kati ya vinara wa ligi, Leicester
City na Tottenham ni alama saba na michezo iliyosalia ni mitatu hivyo
Leicester inahittaji alama tatu kutangazwa kuwa bingwa mpya wa Ligi Kuu
ya Uingereza (EPL) 2015/2016.
0 comments :
Post a Comment