Rais wa Shirikisho la Soka Nchini  (TFF) Jamal Malinzi akiongoza ujumbe wa maofisa wengine wawili wa shirikisho hilo wamefanya ziara makao makuu ya ofisi za TBL Group zilizopo Masaki jijini ambapo walikutana na mkurugenzi wake Mkuu Roberto Jarrin  na kufanya naye mazungumzo.
Ziara hiyo imeelezwa kuwa ina lengo la kudumisha uhusiano miongoni mwa taasisi hizo mbili hususani katika kuendeleza mchezo wa soka nchini.
Malinzi tbl 11
Mkurugenzi Mkuu wa TBL GROUP  Roberto Jarrin (katikati) akisalimiana na Mjumbe wa Kamati ya TFF, Richard Sinamtwa ,  Kulia ni Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Jamal Malinzi.
Malinzi tbl 6
Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Jamal Malinzi (wa pili kulia ) Katibu Mkuu  shirikisho hilo,  Mwesigwa Selestine (kushoto) na Mjumbe wa Kamati ya TFF Richard Sinamtwa (katikati) wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group Roberto Jarrin (Kulia ) wakati walipofanya ziara ya kikazi ofisini kwake Masaki  jijini Dar es Salaam.
Malinzi tbl 7
Mkurugenzi Mkuu wa TBL GROUP, Roberto Jarrin (wapili kushoto) Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF), Jamal Malinzi (wa pili kutoka kulia) Katibu Mkuu  shirikisho hilo , Mwesigwa Selestine  (kulia) na Mjumbe wa Kamati ya TFF, Richard Sinamtwa (kushoto )wakiwa kwenye picha ya pamoja  wakati walipotembelea katika ofisi za TBL Masaki  jijini Dar es Salaam.