Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Watumbuliwa MAJIPU


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu amewasimamisha kazi watendaji wakuu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya kupisha uchunguzi kuhusu wizi na udanganyifu uliofanywa katika akaunti ya madai ya NHIF mkoa wa Mara.

Taarifa za awali zinaonesha zaidi ya shilingi bilioni 2.9 zimeibwa kwa njia ya udanganyifu kutoka katika akaunti yamadai ya NHIF mkoa wa Mara ambazo zimekuwa zikichukuliwa kidogokidogo kwa kipindi cha miaka mitatu tangu 2013.

Waliosimamishwa ni kaimu mkurugenzi mkuu Michael Mhando, mkurugenzi wa fedha na vitega uchumi Deusdedit Rutazaa, mkurugenzi wa mifumo habari Ally Othman na mkaguzi mkuu wa ndani Anne Maneno.

Waziri Ummy Mwalimu pia ameagiza mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali kufanya uchunguzi maalum wa mfumo mzima wa utoaji madai wa NHIF pamoja na akaunti zake katika mikoa yote ili kubaini ukubwa wa tatizo na hatua kuchukuliwa
.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment