CBE Yatolea Ufafanuzi dhidi ya Tuhuma za Ufisadi chuoni Hapo.



CHUO cha Elimu ya Biashara (CBE) kimetoa ufafanuzi kuhusu tuhuma za ufisadi zilizotolewa dhidi yake na kudai si za kweli, zinalenga kuharibu sifa za chuo hicho pamoja na uongozi wake.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Mkuu wa chuo hicho, Profesa Emanuel Mjema alisema kimembaini mfanyakazi wake anayedaiwa kutoa taarifa hizo katika vyombo vya habari na ametakiwa kujieleza huku taratibu nyingine zikifuatia.

Mjema alisema chuo kimesikitishwa na habari hizo zilizochapishwa na magazeti mawili ya kila siku , zikidai upo ufisadi mkubwa katika chuo hicho.

Alisema wamekuwa wakifanyiwa ukaguzi na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) na hakukuwahi kubainika uchafu na kimepatiwa hati safi.

“…niseme tu tutawashitaki waandishi hawa kwa kutoa taarifa ambazo hazina ukweli wowote,” alisema Mjema na kusema kimetaka magazeti husika kukanusha taarifa hizo."
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment