Waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Wahoji Kuhusu Afya ya Askofu Gwajima


Waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, wamesali Jumapili ya tatu bila kuwapo kwa Askofu wao, Josephat Gwajima,lakini wameshtushwa na taarifa kuwa kiongozi huyo wa kiroho ni mgonjwa na anapata matibabu nje ya nchi. 

Waumini hao walisema wamekuwa wakisikia kuwa askofu wao anatafutwa na Jeshi la Polisi na juzi wamesikia kuwa anapata matibabu nje ya nchi wakati wao hawajatangaziwa rasmi kuhusu taarifa hizo. 

Juzi, Wakili wa Askofu Gwajima, Peter Kibatala aliileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mteja wake hakufika mahakamani kwa kuwa yuko nje ya nchi kwa ajili ya matibabu. 

Askofu Gwajima alitakiwa kufika mahakamani hapo anakokabiliwa na kesi ya kumtolea lugha chafu Askofu Mkuu Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi, Cyprian Mkeha. 

Mbali na taarifa za kuumwa, pia Gwajima anatafutwa na Polisi baada ya kusambaa kwa sauti inayosikika kama yake ikitaka Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete afikishwe mahakamani kwa yote yaliyofanyika katika utawala wake. 

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema jana kuwa atalizungumzia suala hilo leo Jumatatu. 

Katika ibada ya jana, kama kawaida, Mchungaji Adriano Edward hakuwaeleza chochote waumini wa kanisa hilo kuhusu alipo Askofu Gwajima wala hali ya afya yake. 

Mchungaji Adriano alipotakiwa kuzungumzia suala la afya ya Gwajima, alisema kupitia msaidizi wake kuwa hawezi kuzungumza chochote na vyombo vya habari.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment