MTATIRO- HATUMTAMBUI PROF LIPUMBA CUF,HAKUNA MTU WA KUTUPANGIA WA KUTUONGOZA AWE NANI..!!



CHAMA cha Wananchi (CUF), kimegomea hatua ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, ya kumrudishia madaraka ya uenyekiti wa chama hicho taifa, Prof. Ibrahim Lipumba.


CUF ilitoa msimamo wa kumpinga Msajili jana ikiwa muda mfupi baada ya taarifa za kurudishwa kwa Lipumba madarakani kuwafikia. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro, alisema kuwa yuko kikaoni, lakini baadaye akafafanua juu ya msimamo wao kupitia ujumbe mfupi wa maneno kuwa, kamwe hawatambui uamuzi huo kwa sababu kwa katiba yao na kwamba Msajili wa Vyama vya Siasa hana mamlaka ya kumrudisha Lipumba kwenye nafasi hiyo.

Mtariro alisema wanachojua ni kwamba jambo pekee analoweza kulifanya Msajili ni kukishauri chama juu ya masuala mbalimbali ya uendeshaji na si kuwawekea mtu wa kuwaongoza.

“Msajili hana mamlaka hayo. Anachoweza kutoa ni maoni tu,” alisema Mtatiro kupitia ujumbe huo mfupi wa simu yake ya mkononi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment