Msemaji
Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika Ofisi ya Rais (Utumishi
na Utawala Bora), Ruth Mollel ameikosoa Serikali akidai imekithiri kwa
ukiukwaji wa sheria za utumishi.
Katika
taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari jana, Mollel ambaye ni
Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Chadema, amesema ameshuhudia
ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Utumishi wa Umma ya Mwaka 2002 kuhusu
suala la nidhamu kwa watumishi tangu Serikali inayoongozwa na Rais John
Magufuli iingie madarakani.



0 comments :
Post a Comment