Rais Magufuli ametengua uteuzi wa mkurugenzi leo October 18 2016


October 17 2016 iliripotiwa taarifa iliyomhusu Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Emmanuel Mkumbo ambapo ilisema kuwa Mkurugenzi huyo amefikishwa mahakama ya hakimu mkazi Mororgoro kwa mashtaka sita, likiwamo la kutishia kuua.
Sasa leo October 18 2016 taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imesema kwamba Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga Emmanuel Mkumbo. Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga atakayejaza nafasi ya Mkumbo utafanywa baadaye.
Hata hivyo taarifa hiyo ya Ikulu haijaeleza sababu ya utenguzi huo.
img-20161018-wa0049
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment