Lowassa: JPM ameshindwa




John Magufuli, Rais wa Tanzania
John Magufuli, Rais wa Tanzania

EDWARD Lowassa, aliyekuwa mgombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema, Rais John Magufuli ameshindwa kutekeleza ahadi zake, anaandika Faki Sosi.
Amesema kuwa, kilichotarajiwa na wananchi kwenye utawala wake sicho anachokifanya na kuwa, matokeo yake yamekuwa ni maisha magumu kwa wananchi huku ajira zikiota mbawa.
Ametoa kauli hiyo jana ikiwa ni kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kufanyika Uchaguzi Mkuu tarehe 25 Oktoba mwaka jana na baadaye Tume ya Uchaguzi nchini (NEC) kumtangaza Dk. Magufuli kuwa mshindi.
Lowassa kwenye uchaguzi huo alishika nafsi ya pili kwa kupata kura 6,072,848 ambapo Rais Magufuli alitangazwa kushinda kwa kupata kura 8,882,935.
Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema ambaye aliungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwenye uchaguzi huo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari amesema, maisha yamezidi kuwa magumu katika utawala wa Rais Magufuli.
Akitoa tathmini ya mwaka mmoja wa Rais Magufuli madarakani Lowassa amesema, Watanzania walikuwa na matarajio ya kuwa na elimu bora, ajira na uchumi jambo ambalo halijafanyika mpaka sasa.
Amesema kuwa, pamoja kuwepo na ahadi nyingi za Rais Magufuli katika nyanja mbalimbali lakini kinachofanyika sasa sicho kile kilichoahidiwa kwenye kampeni zake.
Ametoa mfano kuwa, pamoja na kuahidia elimu bure lakini inayotolewa kwa sasa sio ile iliyoahidiwa na kwamba, ukosefu wa ajira umeendelea kuwa bomu linalosubiriwa kulipuka.
“Pamoja na kuwepo kwa mafanikio katika baadhi ya maeneo, maisha yamekuwa magumu, ajira imeendelea kuwa bomu linalosubiriwa kulipuka,” amesema Lowassa ana kuongeza “elimu bure iliyoahidiwa sio inayotolewa.”
Amesema kuwa, kuwepo kwa ugumu wa maisha kumesababisha shughuli za kiuchumi kuwa ngumu jambo ambalo limewasukuma wafanyabiashara kufikia uamuzi wa kupunguza watumishi ili kukabiliana na hali hiyo.
Hata hivyo, ameonesha kukerwa na hatua ya serikali kukamata na kuwaweka ndani viongozi wa kisiasa hususani wa vyama vya upinzani.
Amesema kwamba, anapotazama nyuma kwenye uchaguzi huyo, anafarijika kuwaongoza Watanzania kupiga kura na kuungwa mkono jambo ambalo limeonesha matumaini makubwa kwao.
“Naamini nilileta sura na msisimko katika siasa za Tanzania. Nilishirikiana na viongozi wenzangu kuionesha nchi demokrasia maana yake nini?
“Ninapogeuka nyuma na kuiangalia siku ile, nasikia faraja kubwa sana hasa kwa jinsi Watanzania walivyotuunga mkono.”
Tarehe Kama ya leo mwaka Jana, ilikuwa siku muhimu sana kwa watanzania na Mimi binafsi.Niliwaongoza watanzania kupiga kura nikiwa mgombea wa upinzani.

Naamini nilileta sura na msisimko mpya katika siasa za Tanzania.Nilishirikiana na wenzangu kuionesha nchi yetu Demokrasia maana yake ni nini.

Napogeuka nyuma kuingalia siku ile, nasikia faraja kubwa sana hasa kwa jinsi watanzania walivyotuunga mkono na kuonyesha matumaini makubwa kwetu.Ujasiri na ushapavu wa hali ya juu aliyouonesha Mke wangu Regina wakati wa kampeni,ulinipa nguvu kubwa.

Chini ya Mwenyekiti wetu Freeman Mbowe,tuliendesha kampeni za kiungwana kama tulivyoahidi.Upepo ule ulivuma kwa kasi mpaka visiwani ambako Maalim Seif aliporwa dhahiri ushindi.

Kwa mujibu wa Tume isiyo huru ya uchaguzi, tulishindwa uchaguzi ule.Hatutaki kuendelea kuyalilia maziwa yaliyokwisha mwagika ambayo hayazoleki, lakini kile ambacho tulikisema wakati ule kwanini tunataka mabadiliko,hivi sasa kila mtu anakiona.

Pamoja na mafanikio machache katika baadhi ya maeneo lakini maisha yamezidi kuwa magumu, ajira imeendelea kuwa bomu linalosubiri kulipuka,Elimu bure iliyoahidiwa siyo inayotekelezwa,utumishi wa umma umekuwa kaa la moto,.Nasononeka sana nikiona viongozi wanavyoshindana kuwasweka ndani madiwani na viongozi wengine wa kuchaguliwa hasa wa UKAWA.

Nawashukuru sana wananchi kwa imani kubwa waliyoionesha kwangu na UKAWA kwa ujumla.Kumalizika kwa uchaguzi ndiyo mwanzo wa uchaguzi mwengine, kwahiyo mapambano ndiyo kwanza yameanza.Kasi,nguvu, ari na hamasa niliyonayo ni kubwa zaidi kuliko wakati mwengine wowote.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment