Wenger:Tuko Tayari Kumsajili Ozili Na Sanchez Kwa Gharama yeyote.



Klabu ya Arsenal ipo katika hatua nzuri ya kukamilisha mpango wa kuwasainisha mikataba mipya wachezaji wake Alexis Sanchez na Mesut Ozil chini ya ushawishi mkubwa unaoendelea kufanywa na meneja Arsene Wenger.


Taarifa zinasema kuwa, Wenger amependekeza wawili hao wasainishwe mkataba wa miaka miwili, ambayo itakua chachu ya kuanza kulipwa mishahara minono kutokana na kazi nzuri na kubwa wanayoifanya kwa ajili ya maendeleo ya Arsenal tangu walipotua klabuni hapo.

Mwishoni mwa juma lililopita Wenger aliwaeleza waandishi wa habari “Tupo tayari kuvunja benki kwa ajili ya kukamilisha mpango wa kusainiwa kwa mkataba mpya wa Ozil ambao utamuwezesha kupokea mshahara wa Pauni 250,000 kwa juma.”

Hali kadhali kauli kama hiyo aliitoa alipoulizwa kuhusu maendeleo ya mazungumzo kati ya uongozi wa Arsenal na Sanchez.

Wenger kwa sasa anamalizia muda wa mwaka mmoja uliosalia kwenye mkataba wake, lakini amekua na matumaini makubwa ya kuwabakisha wachezaji hao klabuni hapo kwa ajili ya maslahi ya baadae.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment