Wakuu Wa Shule za Dar Ambazo Zimeshika Mkia Matokeo Kidato cha Nne Watumbuliwa


Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne  kwama 2016 yametoka na miongoni mwa Shule 10 zenye Wanafunzi waliofeli zaidi Tanzania, 6 zinatoka Dar es salaam na hiyo imemfanya Mkuu wa wilaya ya kigamboni Hashim Mgandilwa kufanya uchunguzi kwenye hizo shule.

Baada ya uchunguzi wake Mkuu huyu wa wilaya ameagiza kushushwa vyeo kwa Wakuu wa shule mbili za za Sekondari ambazo ni Kidete na Somangila Day na ametoa sababu mbili za kuchukua uamuzi huo.

Amesema sababu ya kwanza ni kufelisha na pili kuna mmoja amepata ukuu wa shule katika namna ambayo ina ukakasi na inaonekana kwa namna moja ama nyingine kuna Watu walimtengenezea kukipata hicho cheo

"Hiyo ilileta mvutano shuleni na baadhi ya Walimu walimuunga mkono na wengine hawakumuunga mkono hivyo ikasababisha Walimu takribani 7 kuihama shule hiyo kwa muda wa miezi miwili hadi mitatu." Amesema  DC Mgandilwa
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment