SIMBA Yashinda Rufaa Yake Dhidi Ya Kagera

KAMATI ya masaa 72 ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF imeipa timu ya Simba pointi tatu baada ya kubaini Kagera Sugar ilimchezesha beki Mohammed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano.

Katika mchezo huo Simba ilifungwa mabao 2-1 kwenye uwanja wa Kaitaba ambapo sasa Wekundu hao wamefikisha pointi 61.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Hamad Yahaya amewaambia waandishi wa Habari kuwa baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimaye kila kitu kimepatikana na Simba imepewa pointi hizo.

“Najua maamuzi haya yatawaumiza wengi na yatawafurahisha wengi pia lakini hiyo ndiyo hali halisi,” alisema Yahaya.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment