Bodi ya mikopo ilivyoshiriki maonesho ya vyuo vikuu Jijini Dar Es Salaam


HESLB TCU 1
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal akipokea maelezo kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kutoka kwa Ofisa wa HESLB Bi. Veneranda Malima katika maonesho ya vyuo vikuu yaliyomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. (Picha na HESLB).
HESLB TCU 2
Ofisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa ELimu ya Juu (HESLB) Bw. Saleko Mandara (kushoto) akimwelekeza namna ya kujaza fomu ya kurejesha mkopo Bw. Suleiman Zidi Hisabu ambaye ni mwajiriwa wa Chuo Kikuu cha Abdulrahman Al-Sumait Zanzibar na mnufaika wa mkopo aliopewa na HESLB. Bw. Hisabu alitembelea banda la HESLB katika maonesho ya vyuo vikuu yaliyomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. (Picha na HESLB).
HESLB TCU 3
Mkurugenzi wa Elimu ya Juu katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof. Sylvia Temu akimkabidhi Ofisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bi. Veneranda Malima cheti cha ushiriki katika maonesho ya vyuo vikuu yaliyomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
HESLB TCU 4
Ofisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bi. Joyce Mgaya (kulia) akijibu maswali ya Bi. Dorah Kusiri, mkazi wa jijini Dar es Salaam kuhusu huduma za HESLB. Bi. Kusiri alitembelea banda la HESLB katika maonesho ya vyuo vikuu yaliyomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
HESLB TCU 5
Ofisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa ELimu ya Juu (HESLB) Bi. Joyce Mgaya (kulia) akimwelekeza Bw. Sheha Semtawa (aliyekaa) namna ya kujaza fomu ya kuomba mkopo kwa njia ya mtandao. Bw. Semtawa alitembelea banda la alitembelea banda la HESLB katika maonesho ya vyuo vikuu yaliyomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mwisho wa kuwasilisha maombi ya mkopo ni Julai 31, 2015. (Picha na HESLB).
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment