Chadema wachuana ubunge Tabora Mjini

Wednesday, July 8, 2015

  Nkupamah blog

WANACHAMA watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wametangaza kuingia katika kinyang’anyiro cha kuomba kuteuliwa katika Ukawa kuwania ubunge jimbo la Tabora Mjini.
 
Walitambulishwa jana katika mwendelezo wa mikutano ya hadhara iliyoandaliwa na uongozi wa chama hicho mkoa ambao jana ulifanyika katika kata ya Mpera katika Manispaa ya Tabora.
 
Wanachama wanaowania kuteuliwa na chama hicho ni Profesa Hamba Makambi, Raymond Maganga, Said Mwakasekela, Furaha Kisanji na Peter Mkufya.
 
Mwanachama mwingine, Rehema Raphael anawania viti maalumu wanawake. Wagombea hao wa chama hicho watachujwa Julai 25 na kubaki mmoja atakayepambanishwa na mwingine kutoka kila chama kinachounda ukawa kabla ya kupatikana mgombea atakayepeperusha bendera ya ukawa kwenye jimbo la Tabora Mjini linaloongozwa na Ismail Rage wa CCM.
 
Mratibu wa Kanda wa Chadema, Christopher Nyamwanji alisema viongozi wasiokuwa na dhamira ya kuwakomboa watanzania ndio wameifikisha nchi pabaya.
 
Alieleza kuwa pamoja na mkoa kuwa na misitu katika maeneo mengi, inashangaza kuona wanafunzi wakikaa chini madarasani.
Nkupamah blog
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment