Dkt Magufuli Mgeni Rasmi Mkesha wa kuiombea amani Tanzania

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste (Tanzania
Fellowship of Churches) Askofu Godfrey Malassy (kushoto) akiongea na
waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo 22 Desemba, katika Ukumbi wa Idara ya
Habari jijini Dar es Salaam kuhusu maandalizi ya Mkesha Mkubwa wa Kitaifa wa
kuliombea Taifa pamoja na dua maaum ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli ambaye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika dua hiyo. Kulia ni Mwanakamati wa Jumuiya hiyo, Mchungaji Olivia
Mallonga.
………………………………………………………………………………………….
Na Shamimu Nyaki MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkesha mkubwa wa kuiombea amani  Tanzania  utakaofanyika Disemba 31 mwaka huu katika uwanja wa Taifa.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Pentekoste (TFC)    Godfrey Malassy alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijin Dar es Salaam, na kuthibitisha  kuwa maandalizi yote yamekamilika ikiwemo kibali kutoka polisi, pamoja  washiriki mbalimbali watakaoshiriki katika mkesha huo.
Askofu Malassy ameongeza kuwa mkesha huo  utakuwa ni kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kuijalia nchi yetu kumaliza Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba mwaka huu kwa amani na utulivu,pamoja na Dua maalum ya kumuombea Mhe. Rais afya njema na utendaji mzuri anaoendelea kuufanya kwa maendeleo ya Taifa letu kwa kuwa mara zote amesisitiza kufanyiwa maombi na watanzania.
“Tutatumia nafasi hiyo kumuombea Mhe.Rais katika kutekeleza jukumu kubwa alilokabidhiwa na  watanzania kuongoza Taifa letu ili aweze kufanikiwa katika hilo.”Alisema Askofu Malassy.
Aidha Mwenyekiti huyo amewataka wananchi wote kutumia siku hiyo kumuomba na kumshukuru Mungu kwa amani iliyopo nchini kwa vile ndio msingi mkubwa wa shughuli za kila siku zinazosaidia kupata kipato na maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
Naye Mch.Olivia Mallonga ambaye ni mjumbe katika kamati ya maandalizi ya Mkesha huo amesema kwamba wao kama wadau   wanaendeleza desturi ya kuliombea Taifa amani ili lisije kutumbukia kwenye machafuko kama nchi nyingine .
“Watanzania wana dini ndio maana wanatumia  imani zao kufanya maombi ili Mungu awalinde na maovu au machafuko yanayoweza kutokea kutokana na sababu yoyote.”Aliongeza Mch. Olivia.
Mkesha huo ni wa 17 tangu ulipoanza kufanyika Tanzania na umeleta mafanikio makubwa ikiwemo kuunganisha watanzania bila kujali imani  zao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment