ZSTC ina fedha za kutosha kununua karafuu zote kwa kwa wakulima bila kuwakopa

mwa1 
Na Ramadhan Ali   Maelezo-Zanzibar 
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biashara la Taifa  Zanz
ibar (ZSTC) Bi. Mwanahija Almasi Ali  amesema Shirika hilo lina fedha za kutosha kununua karafuu zote kutoka kwa wakulima kwa fedha taslimu  na hakuna mpango wa kununua karafu zao
kwa njia ya mkopo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Maisara, Bi. Mwanahija alikiri kuwa  msimu huu wa vuli zao la karafuu limekuwa kubwa kinyume na walivyotaraji lakini  wamejipanga  na wanazo fedha za kutosha.
Taarifa ya Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZSTC imekuja kufuatia baadhi ya wadau wanaojishughulisha na zao la karafuu  kuvumisha kuwa wanapofika vituoni kuuza karafuu hupewa risiti na kutakiwa wakae  siku tatu hadi wiki moja ili wakachukue fedha zao.
“Wananchi wanaojishughulisha na zao la karafuu wanatoa taarifa zisizo sahihi kwa ZSTC kuwa hatuna fedha na wanapokwenda kuuza karafuu vituoni hupewa risiti  na kutakiwa wasubiri wiki moja wapatiwe pesa, taarifa hiyo sio sahihi, ” alisema Bi Mwanahija.
Alisema ZSTC ni Shirika  linalofanya biashara  na linaruhusiwa kwa mujibu  wa sheria kukopa Taasisi za kibenki kwa ajili ya kukidhi gharama za kununulia karafuu kutoka kwa wakulima iwapo msimu wa zao hilo umekuwa mkubwa.
Ameongeza  kuwa iwapo kima cha fedha  watakazokopa kimekuwa kikubwa kupita kiwango kinachokubaliwa na Taasisi za fedha  kukopa wanaweza kutoa taarifa Serikalini  na ikawapa fedha kuendelea kununua karafuu za wakulima.
“Mpaka sasa hivi hatujakuwa na shida ya kukopa kutoka Taasisi za kifedha wala kutoa taarifa Serikalini  kupata fedha za ziada  kwa sababu tunazo  za kutosha na tumejipanga, ”alisisitiza Mkurugenzi Mwendeshaji ZSTC.
Alisema wakati  msimu wa uchumaji karafuu za vuli upo katikati, katika wiki ya kwanza ya mwezi Disemba Shirika limenunua tani 236 za karafuu zenye thamani ya shilingi bilioni 3.3 , wiki ya pili tani 379.7 zenye thamani ya shilingi  bilioni 5.315 na  wiki ya tatu wamenunua  karafuu zenye thamani ya shilingi bilioni 7.2.
Kuhusu kuliendeleza  zao la karafuu Zanzibar,  Bi. Mwanahija Almasi alisema Serikali  kwa kutambua umuhimu wa zao hilo imeanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Karafuu ambao lengo lake kubwa ni kutoa visaidia kwa wakulima.
Alivitaja visaidizi hivyo kuwa ni pamoja na kuwapatia wakulima miche  bila malipo, kuhamasisha wananchi  kuanzisha vitalu vya miche ya mikarafuu  na kuwapa mikopo  wakulima wakati wa maandalizi ya kuchuma zao hilo .
“Msimu huu wa vuli Shirika limetoa mikopo kwa wakulima wa karafuu 126 Unguja na Pemba yenye thamani ya shilingi milioni 34,” Mkurugenzi aliwaeleza waandishi wa Habari.
Akizungumzia mwamko wa wakulima wa karafuu kuweka fedha Benki baada ya kuuza karafuu zao ili kujiepusha  kuibiwa alisema pamoja na juhudi wanazochukua kuwapa taaluma juu ya suala hilo bado muitikio haujawa nzuri kwa wakulima wengi.
Amesema wakulima wengi wa karafuu wanapenda kukaa na  pesa zao majumbani ili kupata urahisi wa kuzitumia  wanapozihitaji pamoja na tishio la tatizo la wizi ambalo katika msimu wa karafuu limekuwa kubwa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment