Msanii mkongwe anaefanya poa kwenye
tasnia ya muziki nchini Chege Chigunda anataraji kuachia video yake mpya
ya kimataifa inayo itwa Sweety Sweety ambayo itarushwa kwenye kituo cha
MTV BASE nyimbo ambayo amewashirikisha wakali wanaosumbua Afrika kwa
sasa Run Town wa Nigeria na Uhuru wa Afrika Kusini.
Akizungumza na mtembezi.com Chege
Chigunda ameshukuru msanii Diamond Platnumz kwa kufanikisha kufanyika
kwa hiyo video kwa kumuunganisha na baadhi ya wasanii wa Afrika Kusini,
ili nyimbo hiyo iweze kutambulika na kupigwa katika vituo vya ndani na
nje ya nchi.
Akizungumzia video hiyo Chege amesema
ni video iliyoandaliwa na muongozaji mahiri Justin Campos ambapo wimbo
upo katika mahadhi ya Afro Pop jambo ambalo anaamini itamfikisha mbali
endapo itapata fursa ya kuungwa mkono na wadau wa muziki nchini.
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments :
Post a Comment